Our Feeds

Saturday, 13 February 2016

Unknown

Arsenal vs Leicester: Gunners kuutafuna mfupa uliowashinda wakubwa wote EPL au Mbwa Mwitu watalipa kisasi?

Viongozi wa Premier League Leicester mpaka sasa wamepoteza mechi mbili katika msimu huu, mara moja kati ya hizo ilikuwa ni kipigo kizito cha 5-2 kutoka kwa Arsenal katika dimba lao la King Power mnamo September 2015. Wikiendi timu hizi mbili zinakutana tena, je Gunners wataweza kuutafuna mfupa mgumu uliowashinda wengi msimu huu?
  Kipigo cha Leicester cha 5-2 vs Arsenal kinabaki kuwa kipigo pekee ambacho Foxes walikubali mbele ya maelfu ya mashabiki wake. Mechi nyingine waliyopoteza msimu huu ilikuwa dhidi ya Liverpool (1-0) @Anfield.
Staili ya ushambuliaji ya Arsenal iliweza kuutumia udhaifu wa Leicester ambao timu nyingi wameshindwa kuutumia. Wakati huo, Claudio Ranieri alikuwa bado hajafanikiwa kupata clean sheet hata moja lakini tatizo hilo la ulinzi limedhibitiwa kwa kiasi kikubwa tangu wakati huo. Kwa kifupi Leicester wameruhusu nyavu zao kuguswa mara 3 katika mechi 8 zilizopita – idadi ambayo Alexis Sanchez aliifanikisha ndani ya dakika 48 tu za mchezo mnamo September.
  Jumapili hii Alexis Sanchez atakuwa fiti 100% jumapili katika mchezo ndani ya Emirates. Mabeki wa pembeni wa Leicester wamebadilishwa, lakini kumbukumbu za manyanyaso ya Sanchez zinaendelea kubaki vichwani mwa ‘MbwaMwitu’ wa Claudio Ranieri.
  Katika mchezo uliopita baina ya wawili hawa, Theo Walcott alianza mbele ya Oliver Giroud na alikuwa mwiba mchungu kwenye safu ya ulinzi ya Leicester, lakini Je Wenger atamuanzisha muingereza huyo? Sio rahisi ukiangalia na ukweli kwamba Walcott hajafunga goli tangu kabla ya Christmas na alifanikiwa kucheza kaa dakika 1 tu dhidi ya Bournemouth.
  Mahrez na Vardy
Hakuna ubishi kwamba hawa wawili ni moja ya nguzo muhimu ya mafanikio ya Leicester msimu huu lakini katika mechi iliyopita dhidi ya Gunners walikuwa na siku mbaya. Wawili hao walizimwa, Mahrez alitulizwa vizuri, alipoteza mipira mara 26, zaidi ya mchezaji yoyote yule kwenye mechi hiyo. Vardy alifunga mara mbili lakini magoli yake hayakusaidia lolote mwisho wa siku – japo alimsumbua sana Marteseker, na hilo linaweza kumfanya Wenger ampange Gabriel wikiendi hii.
Staili ya uchezaji!
Tatizo ambalo linaweza kuwapa presha mashabiki wa Leicester sio wachezaji bali staili ya uchezaji ya Arsenal na mbinu atakazoingia nazo Ranieri.
  Ranieri aliamua timu yake icheze kwa kupishana na Arsenal na hilo likamtokea puani. Kasi na ubora wa wachezaji wa Gunners uliwazidi wale wa Leicester na matokeo yake wakapokea kipigo kizito ambacho kilizidi kumpa Wenger rekodi nzuri mbele ya Ranieri. Arsenal walifanikiwa kupiga mashuti 27 langoni na 12 kati ya hayo yalilenga lango – huku matano yakimpita Kasper Schemichel.
Leicester wana rekodi nzuri ya kupata pointi nyingi ugenini kuliko timu yoyote katika EPL msimu huu, na wamebadilika kiuchezaji tangu walipokutana na Gunners mara ya mwisho – hata hivyo Ranieri anatarajia kuwaanzisha wachezaji 9 kati ya walioanza mechi iliyopita – je watafanikiwa kulipa kisasi, tukutane Jumapili usiku kwa ajili ya matokeo ya mchezo huu muhimu kwenye mbio za ubingwa wa England.

Subscribe to Mtembezi Sports via Email :
Previous
Next Post »