Our Feeds

Wednesday, 13 April 2016

Unknown

ARTETA NA GUARDIOLA HUENDA WAKAKAA BENCHI MOJA



Na Amini Nyaungo

Kuna maisha baada ya kucheza mpira mifano mizuri ipo hata hapa Tanzania japo sio wote wanao fikiria maisha baada ya uchezaji, nenda kamulize Msuva ana lengo gani baada ya kustaafu mpira sijui atakwambia nini? 

Mikel Arteta kukaa benchi moja na Pep Man City
Kiungo na Kapteni wa Arsenal Mikel Arteta imearifiwa na ESPN kuwa mchezaji huyu atajiunga na Manchester City katika Benchi la ufundi ili kutoa huduma katika benchi la ufundi wa timu hiyo.

Guardiola wanamahusiano gani?
Walikutana pale La masia katika Academy ya Barcelona kabla Mikel Arteta kutimka na walikuwa marafiki sana sasa taafira zinasema kuwa Gurdiola anataka kumsogeza Manchester City kutokana na uzoefu wa ligi hiyo.

Arteta ni nani?
Kiungo bora kabisa haswa alipata umaarufu akiwa Everton alicheza vizuri alisajiliwa na Arsenal baada ya kufungwa magoli 8-2 dhidi ya Manchester United 2011 maisha yake Emirate haya kuwa Mazuri sana baada ya kuandamwa na Majeruhi ya mara kwa mara kama ilivyokuwa kwa winga wa Simba Uhuru Suleiman.

Alijiandaa kwa hili?
Baada ya kuona maisha ya uchezaji yanaenda kombo ameamua kusomeshwa na timu hiyo ili afundishe Kikosi cha pili  cha Arsenal na Tayari amepata vyeti hivyo itakuwa Rahisi kuwa kocha. Na huu ndio msimu wake wa mwisho Arsenal kwa mwendo wake wa Majeruhi.

Subscribe to Mtembezi Sports via Email :
Previous
Next Post »