Na Amini Nyaungo
Ulishawihi kuota ndoto na hatimae ndoto ulizoota zina kamilika? kutokea kugombania kutoshuka daraja hadi kukaribia ubingwa wa Ligi kuu ya England kocha wa Leicester City Claudio Ranieri ana haya.
ALIWAZA KUCHEZA NA BARCELONA SIKU MOJA
Kocha huyu wakati timu ina karibia kushuka daraja alisema nitashuka nayo bahati nzuri ikabaki na leo habari kubwa pale Epl ni Leicester City, kocha huyu amesema kuwa anafikiria siku moja kucheza na Barcelona katika michuano mikubwa ambayo huenda Machester United,Liverpool na Chelsea wakabakia majumbani kuitazama katika Television.
"Ni ndoto ambayo kama huwezi kuamini kuwa itatokea yaani Barcelona waje hapa King Power Studium kucheza nasi una amini kuwa Real Madrid,Bayern Munich na Barcelona wanakuja uwanjani kwetu?" Ranieri akiongea kupita Sunday Sports
Ranieri mara zote hana haraka katika mafanikio na huwa anasubiri hadi mambo yakamilike huenda akafanya makubwa kupitia Leicester City.