Na Albogast Benjamin
Soka sasa linahamia China na kama una nafasi ya kuchagua klabu basi fanya sasa ili badae ligi inapokuja kuwa kubwa na wachezaji wa kaliba ya Ronaldo na Messi usije kujuta kwa kutofanya maamuzi mapema.
Si kwa bahati mbaya ni mpango kazi wa rais Jinping wa China inapania kujenga viwanja 60,000 vya Kandanda katika kipindi cha miaka 6 ijayo Viwanja elfu 60 vitakarabatiwa na vingine kujengwa upya.
Hayo ni baadhi ya mapendekezo katika mpango wa kandanda ya China ifikapo 2050 ya kuifanya nchi hiyo iwe kati ya mataifa makuu duniani katika kandanda. wakati idadi ya wachezaji watoto wanaosakata dimba kutimia watoto milioni 50.
Rais Xi Jinping amenukuliwa akisema kuwa angeli furahishwa mno iwapo timu ya taifa ya China ingelifuzu tena kwa kombe la dunia la kandanda na hata kushinda kombe la dunia japo wanampango wa kuandaa hivi karibuni.