Our Feeds

Thursday, 7 April 2016

Unknown

REAL MADRID HOI KWA WOLFSBURG, MAN CITY NA PSG HAKUNA MBABE

Ni kama kutoka kumpiga May Weather K/O kisha pambano la pili unakutana Mohamedi Matumla ana kupiga K/O, hayo yamemkuta Real Madrid baada ya kumfunga Barcelona, Na yeye katika mchezo wa La liga usiku wa jana alikubali kipigo kutoka kwa Wolfsburg  mabao 2-0.

Mkondo wa kwanza Robo fainali ulifanyika usiku wa kuamkia leo ambapo Real Madrid akiwa na BBC yake amekubali kulambishwa oili ya watengeneza magari wa aina ya Wolfsburg magoli 2-0, kwa matokeoa hayo inatakiwa wapate Magoli 3-0 ili wapite hatua inayo fuata ya Nusu fainali vinginevyo watatupwa nje ya michuano hiyo.

Wakati huo huo Manchester City na PSG wote walishindwa kutambiana mara baada ya kutoa sare shufwa ya magoli 2-2 kila mmoja alitaka kutengeneza rekodi, magoli ya City yalifungwa na Fernandinho na  Kevin De Bruyne wakati ya Psg yalifungwa na Ibrahimovic na Rabiot.

Subscribe to Mtembezi Sports via Email :
Previous
Next Post »