Our Feeds

Tuesday, 12 April 2016

Unknown

LOUIS VAN GAAL AKUNWA NA SALAAM ZA ANDY CARROLL


Na Albogast Benjamin

Kocha wa Manchester  United Louis Van Gaal amewaonya wachezaji wake kuwa makini na "Andy Carroll Show" mshambuliaji wa West ham kwenye mchezo wao wa jumatano hatua ya robo fainali kombe la FA.

Andy Carroll alipiga show ya dakika sita akipachika mabao matatu kwenye mchezo dhidi ya Arsenal wikiend iliyopita hivyo Van  Gaal anahofia kutopoteza mechi yake hiyo ambayo inaweza kuwa nafasi ya pekee kutwaa  ubingwa msimu huu kama atafanya vizuri.

"Niliona Andy Carroll show ( dhidi ya Arsenal) ," Mholanzi huyo aliwaambia waandishi wa habari . " Carroll ana sifa za ziada na tuliona hilo kwenye mechi na Arsenal."

Arsenal ina walinzi wazuri lakini tuliona Andy aliwafunga hivyo nasisi sehemu yetu ya ulinzi inabidi kuwa makini na mshambuliaji huyo.

Subscribe to Mtembezi Sports via Email :
Previous
Next Post »