Our Feeds

Wednesday, 13 April 2016

Unknown

LUIS ENRIQUE: BARCELONA NI BORA



Na Amini Nyaungo

Kuwapa Nguvu na hamasa wachezaji ni moja ya kazi kubwa ya kocha wa mpira wa miguu na kiongozi yoyote William Gallas alivuliwa unahodha na kupewa Cesc Fabrigas kwa kukosa utulivu wa uongozi.

Gallas alishindwa kuzuia hisia zake mara baada ya kufungwa badala yeye ndio awatulize wenzake akaanza kulia yeye badala ya kutuliza wenzake,na Fabrigas akapewa beji hiyo kubwa japo umri  ulikiwa mdogo.Ferguson alikuwa ana wafokea wachezaji katika vyumba vya kubadilishia nguo baada ya kipindi cha kwanza.

Kocha bora wa Dunia Luis Enrique amewaweka sawa wachezaji wake mara baada kupoteza Michezo miwili katika ligi na kuweka Rehani Ubingwa wa La liga, leo wana kutana na Atletico Madrid Vicente Caldelon.

"Tunataka tuwaoneshe watu kuwa Barcelona ni bora kwenye mchezo na Atletico Madrid" maneno ya Enrique alipokuwa akiongea na waandishi juu ya mchezo wao.

Manufaa ya kauli hii.

Kauli hii kama ya kujihami baada ya kupoteza katika ligi na ugumu wa mchezo wa leo wa Ligi ya Mabingwa kauli hiyo itaweza kuwa na Manufaa kwa wachezaji wake na Benchi zima la ufundi la timu hiyo.

Subscribe to Mtembezi Sports via Email :
Previous
Next Post »