NAIBU waziri wa Habari, vijana utamaduni michezo na wasanii Mh. Anastazia Wambura ametimiza ahadi yake aliyoitoa kwa Timu ya taifa ya Tanzania Twiga stars ya shilingi laki tatu kwa kila mchezaji endapo watapata goli dhidi ya Zimbabwe.
Akizungumza jijini Dar es Salaam wambura amesema kuwa anawapongeza vijana hao kwa moyo wa kujitoa na kutokata tamaa jamba linalotia faraja na kuakisi mafanikio hapo baadae.
“Kwanza nipende kuwapongeza kwa kutokata tamaa baada ya kufungwa 2-1 hapa nyumbani nikakutana nanyi kuwatia moyo, mkaahidi kufanya vizuri haikuwa kazi rahisI KUPATA Ushindi ugenini mmeonyesha moyo wa kujitoa sana licha ya kuwa hakuna manufaa makubwa mnayoyapata ya kifedha, hongereni sana” alipongeza Wambura.
Wambura aliwaasa wachezaji wa Stars, kuwa mfano wa kuigwa katika jamiiili kuondoa dhana kuwa watoto wakike wanaocheza mpira wa miguu hawana maadili jambo linalokwamisha kwa kiasi kikubwa kididimiza mchezo huo nchini.
“Tumerudi kutoka Zimbabwe na timu imetawanyika japo sio imetawanyika kabisa, hata huku mliko mnapaswa kuendelea na mazoezi, na tubadili mitazamo sisi wenyewe kwanza kuwa mfano wa kuigwa hii itasaidia wazazi kuruhusu watoto wao kushiriki mchezo huu, Watambue kuwa watoto wote wa kie na wa kiume wanapaswa kucheza kwa hiyo kuwe na mgawanyo wa kazi ili kutoa nafasi kwa watoto wote kucheza siyo wakimue peke yao ”. Alishauri Wambura.
Meneja wa timu hiyo Furaha Francis, amewaomba wadau wamchezo huo kuwaunga mkono kwa kuziwezesha timu zote za wanawake na wanaume, huku akishauri Serikali kuzisimamia timu za taifa walau kwa 50% ili kulisadia Shirikisho la soka nchini TFF ambalo wakati mwingine huzidiwa kutokana na kuwa na bajeti ndogo.
Kepteni wa timu hiyo Amina Rashid, ameshauri kuanzishwa na kuboreshwa kwa ligi za soka za wanawake ili kuepuka malalamiko ya mara kwa mara kuwa timu hiyo haifanyi vizuri.Naye Mlinda lango wa timu hiyo Fatuma Omary amesemakuwa ni vema kuwekeza katika soka la vijana wadogo wa kike ili kuwezesha upatikanaji wa wachezaji pale wanapohitajika.
“Ukiwa na wachezaji wadogo waliandaliwa mapema hata tunapocheza sisi tunakuwa tunajuwa baadae kuna wadogo zetu watakuja kushika na nafasi zetu sio kila siku Amina na Fatuma wasipo kuwepo kocha anawaza ataziba vipi pengo lake”
Twiga ilifungwa na Zimbabwe 2-1 jijini Dar es Salaam katika mechi ya awali na kisha kutoka sare ya bao 1-1 katika mechi ya marudiano iliyochezwa nchini Zimbabwe mapema mwezi uliopita ikiwa ni mechi za kuwania kufuzu kwa kombe la mataifa ya Afrika.